Friday, February 8, 2013

MKUTANO MKUU WA NNE WA JUKWAA LA WAKRISTO TANZANIA (TCF)


TANZANIA CHRISTIAN FORUM (TCF)
MKUTANO MKUU WA NNE WA JUKWAA LA WAKRISTO TANZANIA (TCF)

TAMKO RASMI
“ATUKUZWE MUNGU JUU MBINGUNI, NA DUNIANI IWEAMANI KWA WATU ALIOWARIDHIA”

Utangulizi
Katika Mkutano Mkuu wa Nne wa Jukwaa la Wakristo Tanzania, Tanzania Christian Forum – TCF, uliofanyika katika Kituo cha Mikutano na Mafunzo cha Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Kurasini jijini Dar es Salaam, tarehe 6 Desemba, 2012; Wajumbe walitafakari kwa undani juu ya kuzorota kwa mahusiano baina ya Dini mbili za Ukristo na Uislamu nchini Tanzania, pamoja na kutathmini juu ya wajibu wa Kanisa na Utume wake wa Kinabii kwa taifa letu.

Jukwaa la Wakristo Tanzania (TCF) linajumuisha taasisi kuu za Umoja wa Makanisa nchini kama ifuatavyo;-
Jumuiya ya Kikristo Tanzania - CCT
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania - TEC
Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste Tanzania - PCT
Kanisa la Waadventisti Wasabato – SDA (observers)


Tafakari
Tafakari yetu ilianza kwa kujiuliza yafuatayo:

1.      Ni mwenendo gani uliotusibu hivi karibuni kusababisha kukutana kwetu hapa?
Vikundi vya kihalifu vikiongozwa chini ya mwavuli wa waamini wa Kiislamu vimekuwa vikishambulia kwa ukali na kikatili sana imani, mali, majengo na makanisa ya Wakristo kwa jeuri na kujiamini.

2.      Kwa mwenendo huo ni kitu gani kilicho hatarini?
Vitendo na mienendo yote ya namna hiyo inahujumu sana Amani, Mapatano na Uelewano kati ya watu wote  nchini mwetu. Tunaelewa kwamba ni waamini wachache tu wenye kutenda maovu hayo, lakini mienendo ya kikatili ya namna hii huchochea shari miongoni mwa walengwa wa ukatili husika na kutaka kulipiza kisasi hata kusababisha uvunjifu wa amani.

3.      Ni athari gani kwa nchi, katika muda ujao, iwapo mienendo hiyo haitadhibitiwa na kukomeshwa kabisa?
Katika nyakati zetu hizi, tunashuhudia fadhaa na migogoro mingi ya kijamii. Kuna hasira kubwa ya chinichini inayotokana na kasoro nyingi za kiutendaji katika mihimili mikuu ya uongozi na utando mkubwa wa ufukara wa kutupwa kwa wananchi wengi usio na matumaini ya kumalizika hivi karibuni. Hatari ya hali hii ni dhahiri kwamba makundi nyemelezi (kisiasa, kiuchumi na kidini), kwa kutumia vikundi halifu vilivyo katika hali ya ufukara na migogoro, yatavielekeza kimapambano na kiharakati kutetea kijeuri ajenda hasimu za wale walio madarakani au washindani wao kwa maslahi ya wanyemelezi. Hali tunayoelezea sio ya kufikirika kwani ndiyo inayotokea huko nchini Nigeria, Kenya na nchi za Afrika ya Kaskazini hivi sasa. Tanzania haina kinga ya kipekee kuiepusha kukumbwa na maovu ya namna hiyo bila utaratibu na vyombo thabiti kuhimili mienendo hasi kama hii. Kutokana na matukio na kauli zinazotolewa na watu mbalimbali hapa nchini, inawezekana tayari wanyemelezi wako kazini wakiongoza vikundi kusukuma ajenda za kutekeleza maslahi yao.

CHRISTIAN PERSECUTIONS: TANZANIA RANKED AMONG 50 MOST DANGEROUS

Tanzania has been, recently, mentioned among the countries where Christian Persecution rate is shooting up. For many years, Tanzania is mentioned among the peaceful countries.

The weekly Christian newspaper in Swahili "NYAKATI" (Times), of February 3rd-9, 2013, reported that Tanzania ranked 24th among 50 most dangerous countries on Christian Persecution.
The reason for this rise, is due to the increase of radical Muslims in many African countries, the report said.

Radical Muslims are struggling to impose Islamic laws (sharia) to change the secular state into Islamic territory, which ranges politically, economically and socially.

RELIGIOUS PREFERENCE:SOURCE OF FRACAS BETWEEN CHRISTIANS AND GOVERNMENT IN TANZANIA

Religious preference on the meat processing, has, once again, caused the fracas between the Christian community on one hand and the Tanzania government on the other hand.
This happened on January 12, 2013 at Nyehunge village, Sengerema District in Mwanza region, 1154 km from Dar es Salaam, where, the Mwanza Regional Commissioner,  Evarist Ndikilo, accompaned by Police officers, banned Christians to slaughter animals for their food, and ordered that the whole process must be done by Muslims only. He further warned to take severe action to any Christian who would go against the order.His biased and unconstitutional order, made Christians angry and furious as a result, they left the meeting place and dispersed, leaving the RC with just few people.

RC Ndikilo, warned Christians that they should not dare slaughter animals, but must submit under the Islamic laws of slaughtering animals. Islamic  laws demand that, an animal must face towards the Kaaba in Mecca, during slaughtering exercise, the direction  towards which all Muslims worldwide face during prayers.

Earlier, the African Inland Church Pastor, asked the RC how Islamic tenets are forced  into the Christian community, and inquired to know if the country is an Islamic state, to which the RC arrogantly replied: Dont you know!

The exercise, apart of undermining the Christian faith while promoting Islamic as superior, Non-Muslims are charged tsh.2000/- (US 1.24) per  every single cow, and tsh.1000/- for each goat and sheep (US 60p), and chicken tsh.500/=.