Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Absalom Mwakyoma, alithibitisha kuwapo kwa tishio hilo lakini alikataa kuzungumzia zaidi kwa madai ni la kiusalama zaidi. 


“Hilo jambo lipo lakini sitalizungumzia, kwani ni mambo ya kiusalama zaidi…wewe nani amekupa taarifa hizo, muulize aliyekwambia akufafanulie,” alisema. 


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Mtendaji Utawala wa Kiwanda cha Sukari cha TPC, Jaffary Ali, wamepewa taarifa za kuchukua hadhari juu ya kuwapo kwa tishio la shambulio kiwandani hapo.